Christian Eriksen alifunga bao sekunde ya
11 tu ya mchezo, bao la Eriksen ndio linakuwa bao la mapema zaidi kwa
Manchester United kuwahi kufungwa katika ligi kuu ya EPL.
Lakini nlinzi wa Manchester United
Phill Jines akijifunga bao lililoufanya mchezo kuisha kwa Tot kushindwa
kwa bao 2 kwa 0 na sasa Tot wanakuwa wamefaidika kwa mabao 3 ya
kujifunga ndani ya msimu huu.
Ushindi wa leo wa Tottenham mbele ya
United unawafanya Tottenham Hotspur kwa mara ya kwanza baada ya miaka 52
iliyopita kuwafunga Manchester United katika michezo mitatu nyumbani
kwao.
Wakati United wakifa, majirani zao
Manchester City waliibuka na ushindi wa mabao matatu huku mabao ya leo
yakiwafanya kuwa timu ya kwanza barani Ulaya kufunga mabao 100 msimu
huu.
Mchezaji mpya wa Everton Theo Walcotta
lifunga mara mbili wakati Everton ikiichapa Leicester bao 2 kwa 0 huku
Chelsea wakiwa nyumbani wakakubaki kipigo cha mabao 3 kwa nunge toka kwa
Afc Bournamouth.
Newcastle wakiwa nyumbani walilazimishwa suluhu ya bao moja kwa moja
dhidi Burnley, Stoke City na Watford nao wakamaliza mchezo wao kwa sare
ya kutokufungana.
0 maoni:
Chapisha Maoni