Mchezaji wa zamani na kiongozi wa
timu ya mpira wa miguu wa nchini Uingereza David Beckham amefanikiwa
kuzindua mpango wake wa muda mrefu wa uzinduzi wa timu yake ya soka huko
Miami.
Beckham alichungulia fursa hiyo katika harakati za kufunga mkataba timu yake ya zamani ya LA Galaxy mwaka 2014.
Timu
hiyo haijatajwa mpaka sasa ingawa inatarajiwa kucheza mbele ya umati
wa watu elfu ishirini na tano mjini Overtown na katika viwanja vilivyoko
karibu na mji huo.
"ninafuraha kubwa kuileta timu hii kubwa
kwenye jiji hili kubwa, ilikuwa ni safari ndefu na ngumu mpaka kufikia
hapa nilipo leo anasema kiungo wa zamani wa timu ya Manchester United
Beckham, mwenye umri wa miaka 42.Nina waahidi itakwenda katika ligi
ikiwa ni timu bora anajinasibu David.
Baada ya uzinduzi huo David
Bekham alipongezwa na watoto wake wanne kwa njia ya video maalum akiwemo
mkewe Victoria, ambaye aliwahi kuwa mwanamuziki wa zamani wa kundi la
Spice Girl , mshindi mara 23 wa michuano ya Grand Slam Serena Williams,
mshini mara nane wa medali ya dhahabu wa michuano ya Olimpic Usain Bolt
na watu wengine maarufu akiwemo Brady, Will Smith, Jay Z na Jennifer
Lopez.
Bekham akiwa katika klabu ya Real Madrid enzi alipokuwa akiitumikia |
Beckham, alijiunga na timua ya LA Galaxy akitokea timu ya
Real Madrid mnamo mwaka 2007, na kuwa mchezaji wa kwanza mstaafu
kumiliki timu katika ligi.
Anajinasibu David kuwa alijiunga na timu ya Galaxy kwasababu
alitambua uwezekano wa kudumu kwa muda mrefu katika ligi hii, "alisema.
Niliamua
kuondoka Real Madrid na kwenda kwenye ligi ambayo ilikua inasuasua,
ilikuwa ni hatua kubwa mno niliyopiga na kitu kimoja ninachokijua ni
kuwa hatua hiyo itazaa matunda yenye changamoto lakini changamoto zenye
kusisimua.
Kamishna Garber alikuja akaketi karibu yangu na kuanza
kunieleza mipango ya ligi na wapi anapotaka kuifikisha nilikuwepo tangu
siku ya kwanza.
Uzinduzi huu haikuwa kazi rahisi kwa muda wa
miaka minne ya utafutaji kiwanja eneo la kusini mwa Florida huku
tukipingwa na baadhi ya watu katika maeneo kadhaa.
Washirika wa
David Beckham walinunua ardhi tayari kwa kujenga uwanja wao mnamo
mwishoni mwa mwaka 2015, baada ya kushindwa mara tatu kununua eneo
walilolitaka na bora zaidi kwa shughuli hiyo.
Serikali ya Miami
ilifikishwa mahakamani na mfanyabiashara tajiri Bruce Matheson, aliyedai
kuwa timu ya Beckham ilinunua ardhi haikununua kwa gharama stahiki na
zabuni isiyokuwa na ushindani bila kufuata utaratibu. Madai hayo
yalitupiliwa mbali, ingawa mfanya biashara huyo Matheson ameapa kukata
rufaa.
Washirika wa Beckham ni pamoja na meneja wa zamani wa kundi
la Spice Girls Simon Fuller, Mfanya biashara mwenye asili ya Bolivia na
Marekani Marcelo Claure, Mfanya biashara kutoka Florida Kusini Jorge ,
Jose Mas na Mjasiriamali wa Kijapani JMasayoshi Son.
0 maoni:
Chapisha Maoni